Raheem Sterling, winga wa Uingereza, kwa sasa anazidisha sintofahamu juu ya mustakabali wake katika klabu ya Chelsea. Kukosekana kwa mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 29 kwenye kikosi cha mechi ya kwanza ya msimu huu kumezua maswali kuhusu hali yake katika klabu hiyo.
Katika taarifa iliyotolewa muda mfupi kabla ya kuanza, wawakilishi wake walielezea haja ya ufafanuzi. Akizungumza katika mkutano na waandishi wa habari baada ya mechi hiyo, kocha mkuu Enzo Maresca alipoulizwa kuhusu uwezekano wa Sterling kuichezea klabu hiyo mara baada ya dirisha la usajili kukamilika.
“Sijui. Ninachoweza kusema ni kwamba ulikuwa uamuzi wa kiufundi kutocheza Sterling, na kwamba kesho, pengine, tutaangalia kukaa chini na kufafanua hali hiyo, lakini hakuna kingine zaidi ya hilo,” Maresca. alisema.
“Wachezaji wote, kwa sasa, ni wachezaji wa Chelsea. Iwapo watabaki kuwa wachezaji wa Chelsea basi tutajaribu kuwatumia, lakini ni uamuzi wa kiufundi tu, hakuna zaidi.”
“Namtaka Raheem Sterling, lakini pia nataka wachezaji 30 tulionao. Hata hivyo, hakuna nafasi kwa wote. Kwa hiyo baadhi yao watalazimika kuondoka.”
Kikosi cha sasa cha The Blues kina wachezaji 42, na hivyo kuzua maswali kuhusu hitaji la harakati za kupunguza kikosi. Sterling alijiunga na Chelsea mwaka 2022 akitokea Manchester City na kucheza mechi 81 na kufunga mabao 19.
Hali hii ya sintofahamu kuhusu mustakabali wa Raheem Sterling katika Chelsea inaonyesha maendeleo na marekebisho yanayohitajika ndani ya timu ili kuhakikisha ufanisi wake na mafanikio ya kimichezo. Wafuasi wamesalia wakisubiri ufafanuzi zaidi kuhusu nafasi ya mchezaji ndani ya timu na mustakabali wake katika klabu.