Katika kambi ya Deir al-Balah, katikati mwa Ukanda wa Gaza, watu wazima na watoto wanakimbilia kupata sehemu ndogo ya chakula. Tangu Oktoba 7, Shirika la Chakula na Kilimo la Umoja wa Mataifa, pamoja na mashirika mengine, yameandika uharibifu wa mfumo wa chakula wa eneo hilo, ikiwa ni pamoja na mashamba na uvuvi.
Maisha hapa ni magumu sana. Tuliteseka katika maeneo yote, iwe ni kutoa nailoni, hema, maji au chakula. Leo tunapokea chakula kwa njia ya hisani, ambayo siku zingine sio nzuri. Lakini tunamshukuru Mungu, hali yetu ni bora kuliko ya wengine.
Maji yanapatikana kwa saa moja, kisha kuzima kwa saa moja. Mwaka mzima wa mateso, mateso ambayo Mungu pekee ndiye anajua.
Katika mzozo ambao umewaacha wakazi wengi wakiwa maskini, michango ya chakula hutoa njia ya kuokoa maisha.
Hata hivyo, Israel inaruhusu tu malori ya misaada kupita katika sehemu tatu za vivuko, ikiwa ni pamoja na mbili ndogo kaskazini mwa eneo hilo na moja kusini, Kerem Shalom.
Wataalamu wa Umoja wa Mataifa walisema mwezi Julai kwamba “njaa hiyo imeenea kutoka kaskazini mwa Gaza hadi katikati na kusini.”
Kwa mujibu wa shirika la habari la Palestina Wafa, operesheni ya Israel katika ardhi hiyo iliua Wapalestina 41,431 na kuwajeruhi wengine 95,818.
Miezi kadhaa ya mazungumzo ya kusitisha mapigano yameshindwa kuleta muafaka kati ya pande zinazozozana.
Mashtaka ya “kampeni ya njaa”
Mtaalamu huru wa Umoja wa Mataifa kuhusu haki ya chakula ameishutumu Israel kwa kuendesha “kampeni ya njaa” dhidi ya Wapalestina wakati wa vita vya Gaza, madai ambayo Israel inakanusha vikali.
Katika ripoti iliyosambazwa Septemba 4, mpelelezi Michael Fakhri alisema ilianza siku mbili baada ya shambulio la kushtukiza la Hamas kusini mwa Israel na kuua takriban watu 1,200, wakati shambulio la kijeshi la Hamas Israeli lilipozuia chakula, maji, mafuta na vifaa vingine Gaza.
Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu alisema shutuma za Israel kuzuia misaada ya kibinadamu ni “uongo wa aibu.”
Mapema mwaka huu, Mahakama ya Kimataifa ya Haki iliiamuru Israel kudhamini msaada wa chakula “bila kuzuiliwa” kwa Gaza.
Kufuatia shinikizo kubwa la kimataifa, serikali ya Netanyahu hatua kwa hatua imefungua sehemu kadhaa za kuvuka kwa usafirishaji unaodhibitiwa madhubuti. Fakhri alisema msaada huo mdogo ulikuwa unaenda hasa kusini na kati ya Gaza, na sio kaskazini ambako Israel iliwaamuru Wapalestina kwenda.
“Mwezi Disemba, Wapalestina huko Gaza waliwakilisha 80% ya watu duniani wanaokabiliwa na njaa au janga la njaa,” Fakhri alisema.. “Kamwe katika historia ya baada ya vita hakuna idadi ya watu waliokufa njaa haraka na kabisa kama ilivyokuwa kwa Wapalestina milioni 2.3 wanaoishi Gaza.”
Profesa huyo wa chuo kikuu anasema ilianza mwaka 1948 na Israel kuendelea kuwahamisha Wapalestina. Tangu wakati huo, ameishutumu Israel kwa kupeleka “mbinu mbalimbali za njaa na njaa dhidi ya Wapalestina, kuboresha kiwango cha udhibiti, mateso na kifo kinachoweza kusababisha kupitia mifumo ya chakula.”